DHAMIRA:
-Katika ufahamu (wa mtu) Mwanadamu
kuna jambo fulani linalofanya kazi kama hakimu / wa maadili.Linawaambia watu
mambo yaliyo mema na mabaya.Linawahimiza watu kufanya mema,nalo lina
wahakikishia kama wamefanya mema au kama wana hatia,kufuatana na kutii au
kutotii sauti hiyo ya ndani.Hakimu huyu wa maadili ndani yetu huitwa dhamiri.
Kwa ufupi dhamiri ni ile hali ya kuona jambo
au kusikia na kufikiri yale unayofikiri
na kutaka kuyatendea kazi./ dhamira inafanya kazi ya kupima na kuchuja na kisha
kukuruhusu kufanya au kutenda. Unapofanya kwa wakati sahihi na mahali sahihi
unapata amani na unapokosea unajisikia hukumu au hatia hiyo ndiyo kazi ya
dhamira au kukukataza usifanye.
Rumi
2:15 – 16.”Hao waionyesha kazi ya torati iliyo andikwa moyoni mwao dhamiri
yao ikiwashuhudia na mawazo yao wenyewe kwa wenyewe yakiwashitaki au
kuwatetea; Katika siku ile Mungu atakapozihukumu,sawasawa na injili yangu kwa
Kristo”.
1 Yohana 3:19-20
“Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wakweli nasi tutaituliza mioyo yetu mbele
zake ikiwa miyoyo yetu inatuhukumu kwa maana Mungu ni mkuu kuliko miyo yetu,
naye anajua yote.Wapenzi mioyo yetu isipo tuhukumu tuna ujasiri kwa Mungu”.
Katika agano la kaleinaeleza wazi inavyo fanya kazi. Mwanzo 3:7-8 “Wakafumbuliwa macho wote
wawili wakajijua kuwa uchi wakashona majani ya mti wajifanyia nguo; Kisha
wakasikia sauti ya Bwana Mungu akitembea bustanini wakati wa jua. Kupunga
Adamuna Mkewe wajificha kati ya miti ya bustani Bwana Mungu asiwaone.
Kilichofanya Adamu na Mkewe wakajifiche. “Kilicho fanya Adamu na Mkewe
wajifiche baada ya kusikia sauti ya Mungu ni ile hali ya dhamira ya mioyo yao ikiwaambia wamekosea
na kujisikia hukumu.Kutokana na dhamira walijiona hawastahili kuonana na Mungu.
Ayubu 27:6 Haki
yangunaishika sana
wala sitaiacha.Moyo wangu hauta nisuta
wakatiniwapo hai. Dhamiri inajulisha makosa yako ungali bado uko hai na
dhambi zako.
Daudi alijua makosa yake kwasababu dhamira ilimwambia.
Zaburi51:3-4
Maana nimejua mimi makosa yangu na dhambi yangu imbele yangu daima. Nimekutenda
dhambi wewe peke yako na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa
una, haki unenapo. Na kuwa safi
utoapo hukumu.
-Kumbuka kuwa nia ni tofauti na dhamira lakini zinafanya
kazi katika wakatimmoja.
-Mara nyingi watu wamekuwa wakipuuzia sauti ya ndani,
matokeo yake wanajikuta wameangukia kwenye dhambina, baada ya hapo dhamira bado
itasimama kuku hukumu. Kuwa umekosea unastahili adhabu.
JINSI GANI DHAMIRA
INAWEZA KUFA / KUCHAFUKA:
1.Kwa kutojali sauti
ya dhamira inapo mshauri na kutoa hukumu. Nia inapo kataa ushauri na hukumu ya
dhamira na kuamua kufanya kile nia inachoona / kusikia bila kujali kutatokea
nini baada ya kutenda au kutotenda, mf.Kabla Adamu na Hawa hawaja muasi Mungu,
nia pamoja na dhamira zilikuwa safi
zilisikilizana.
Nia ilikubali kile dhamira inachosema. Dhamira ilisimamia
kuwa muamuzi mzuri.
Hawa alipo kubali kumsikiliza shetani na kuruhusu msukumo
mkubwa wa nia ya shetani kugeuza nia
yake,hatimae aliweza kupuuzia Makatazo
ya dhamiri bila kujali kutokea nini?
Hapa ndipo dhamira
ilipoanza kuharibika, unapoona mtu ana rudia-rudia dhambi hiyo mara kwa mara
ujue dhamiri yake imekafa juu ya hukumu ya dhambi hiyo huona tu ni jambo
la kawaida kwake hata kama
ataambiwa ni dhambi kwake yeye hakiri kuwa ni kosa.
2. KUFA KWA DHAMIRA:
Dhamira inaweza kufa baada ya machafuko / kuchafuliwa bila
kufanyiwa matengenezo ya usafi wa kweli wa kusikilizwa, na kufuta hatia zilizo
moyoni; kwa damu ya Yesu Kristo. Mf. Tito
1:16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu bali kwa matendo yao wanamkana,ni wenye machukizo,waasi,wala
kwa tendo jema hawafai.
Inafikia mtu analisoma Neno na anafanya tofauti na Neno na
hajisikii hukumu. Kwa sababu dhamiri ilisha kufa kwa kutosikilizwa.
Kwa nini? Nia na dhamira kupingana? Nia na dhamiri hupingana
kwasababu ya kukosa Neno ndani yake. Nia itafikiri sawa na Neno.Dhamira
itahukumu sawa na Neno hapo hupata majibu yaliyo sahihi. Wakati mwingine
dhamiri hupingana hapo mtu hujisikia kufanya jambo au kutofanya, kusita sita
moyoni mwake.
DHAMIRA INAPO KUWA SAFI:
Dhamira iliyoendelea vizuri katika usafi humwongoza mtu ili
ifanye mambo mema, haidhuru kama yameandikwa
katika sheria fulani fulani au sivyo.
Rumi 13:5 Kwa
hiyo ni lazima kutii. Si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya
dhamira, inafikia mahali tunaacha kufanya dhambi si kwasababu ya hukumu ya
Mungu bali kwa sababu ya dhamiri safi
ndani yetu ya kumpenda Mungu.
-Utaamua kwa busara na utafikiri kwa busara na kufanya kwa
busara, bila upinzani.
1 Petro 3:16
Nanyi mwe na dhamiri njema. Ili katika Neno
lile mnalosingiziwa.Watahayarishwe wale wautukanao Mwenendo wenu mwema katika
Kristo.
FAIDA
Faida ya dhamiri na nia vikiwa,
vime safishwa na kujaa Neno la Mungu.Utaweza kupambanua safi ya shetani na ya Mungu.
Kolosai 3:16 Neno
la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu
katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana. Kwa saburi na kwa nyimbo na
tenzi za Rohoni huku mkimwimbia Mungu
kwa Neema Miyoyoni mwenu.
Maana yake kila matakalo kufanya lita kuwa sawa na Neno, na
kila mtakalo tenda mtatenda sawa na Neno. Na kila mtakalosikia au kuona
mtafanya sawa na Neno.
Kolosai 3:17
Nakila mfanyalo kwa Neno au kwa tendo, fanyeni yote kwa jina la Bwana Yesu,
Mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.
MAMBO YA KUTAMBUA:
KATIKA KUWA SAFI;
KATIKA DHAMIRI:-
- Kuna watu wanajisikia hukumu hata kama wametubu bado wanajisikia hawaja samehewa. Ni lazima waamini kuwa wamesamehewa, maana msamaha hutoka kwa njia ya imani kukiri mbele za Yesu na kuacha dhambi.
- Wajisamehe wao wenyewe binafsi kwa makosa waliyotenda katka nafsi zao na dhamiri zao. Kukiri na kuacha kujitendea nafsi zao mabaya.
- Waamini kuwa wamejisamehe na wao wamesamehewa la sivyo wataona hawaja samehewa, na pia ni ngumu kwao kuwasamehe wengine. Na wao kupokea msamaha.
- Kama mwanadamu ni lazima utambue kwamba una dhamiri safi, si lazima kuwa bila kosa ishi kwa unyenyekevu hata kama dhamiri yako ina kushuhudia huna kosa endelea kuishi maisha ya usafi, usijihesabie haki. 1.Kor 4:4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini nisi hesabiwe haki kwa ajili hiyo; Ila anihukumuye mimi ni Bwana.
- Dhamiri ni taa au jicho la kupambanua mema na mabaya, Kwa hiyo dhamiri yako inatakiwa kuwa safi Mbele ya Mungu wala siyo safi kwa kadiri ya taratibu au kanuni ambazo umejipangia mwenyewe.
-Dhamiri ikiwa chafu na mwili wako
huwa mchafu / huwa giza.
Luka 11:34 -36 Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote unao mwanga, lakini likiwa bovu
mwili wako nao una giza.
Angalia basi, mwanga ulio ndani yako usije ukawa giza. Basi kama mwaga umeenea katika mwili
wako wote, wala hauna sehemu liyo na giza mwili
wako wote utakuwa na mwanga mtupu; kama vile
taa ikumulikapo kwa mwanga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni